Hadithi: Mwanafunzi Mchawi - Sehemu ya Pili
Mtunzi: Than JM
Ilipoishia sehemu ya kwanza kama hukuisoma pitia blog ipo hapa hapa
.....Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke yake nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....
Sehemu ya pili
...DOREEN aliendelea kuongea maneno aliyoyajua mwenyewe akiwa bado yupo uchi wa mnyama nyuma ya bweni alilokuwa anaishi.
Ghafla kipande kidogo cha karatasi nyeupe kikashuka mikononi mwake bila kuonekana kilikotokea. Doreen alicheka kwa sauti kali ya kutisha sana kisha akalikazia macho karatasi lile, matone ya damu yaliangukia kwenye karatasi lile kutoka kwenye macho yaliyotisha sana ya Doreen kwani yalikuwa na rangi nyeusi halafu yakawa na umbile kama macho ya paka.
"Nenda mpaka ofisi ya mkuu wa shule ukamalize kazi." alisema Doreen akiwa amelinyanyua karatasi like kwa mkono wake wa kushoto. Karatasi likatoweka mkononi mwake na kupepea kwa nguvu kama vile limerushwa na upepo mkali.
Doreen alipomaliza kazi hiyo akasimama vizuri kama mwanajeshi aliyejipanga kwaajili ya gwaride kisha akainamisha kichwa chake chini akapotea eneo lile.
****
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mabango walikuwa wanahofu kubwa sana kila wakikaa walifikiria kifo tu. Usingizi haukuwajia hata mara moja hivyo usiku waliketi makundi makundi wakizungumza hili na lile.
Wakati huo Dorice rafiki kipenzi wa Doreen alikuwa amejitenga pembeni akizungumza na mpenzi wake aitwaye Eddy, kijana mtanashati, mzuri, mpole na akili nyingi sana darasani.Wasichana wengi shuleni pale walitamani kuwa nae lakini bahati ilimwangukia Dorice pekee.
"Eddy unajua naogopa sana.." ilikuwa sauti ya Dorice akiwa amemkumbatia Eddy kwani kigiza kile cha usiku kiliwaficha wasionekane hivyo wakajiachia.
"unaogopa nini Dorice mpenzi wangu?"
"Naogopa kufa!" binti Huyo wa kinyaturu, mrembo aliyeumbika aliongea kwa sauti ya madeko sana.
"siku zote nakwambia Dorice kama Mungu alipanga huwezi kupangua , mwanadamu asikutishe kwa lolote. Huyu anayeua wenzake naye ipo siku yake tu maana hakuna atakae bakia milele na mwisho wa maji ni tope!"
"Najua mpenzi wangu ila hali kiukweli inatisha sana"
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mabango walikuwa wanahofu kubwa sana kila wakikaa walifikiria kifo tu. Usingizi haukuwajia hata mara moja hivyo usiku waliketi makundi makundi wakizungumza hili na lile.
Wakati huo Dorice rafiki kipenzi wa Doreen alikuwa amejitenga pembeni akizungumza na mpenzi wake aitwaye Eddy, kijana mtanashati, mzuri, mpole na akili nyingi sana darasani.Wasichana wengi shuleni pale walitamani kuwa nae lakini bahati ilimwangukia Dorice pekee.
"Eddy unajua naogopa sana.." ilikuwa sauti ya Dorice akiwa amemkumbatia Eddy kwani kigiza kile cha usiku kiliwaficha wasionekane hivyo wakajiachia.
"unaogopa nini Dorice mpenzi wangu?"
"Naogopa kufa!" binti Huyo wa kinyaturu, mrembo aliyeumbika aliongea kwa sauti ya madeko sana.
"siku zote nakwambia Dorice kama Mungu alipanga huwezi kupangua , mwanadamu asikutishe kwa lolote. Huyu aneua wenzake ipo siku yake tu!"
Akashtuka kidogo halafu akaichukua ili aisome vizuri. Mwalimu Mbeshi hakutaka kuamini kile alichokiona, akataharuki kwa hofu na mshangao mkubwa
ITAENDELEA SEHEMU YA TATU
Mtunzi: Than JM
Ilipoishia sehemu ya kwanza kama hukuisoma pitia blog ipo hapa hapa
.....Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke yake nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....
Sehemu ya pili
...DOREEN aliendelea kuongea maneno aliyoyajua mwenyewe akiwa bado yupo uchi wa mnyama nyuma ya bweni alilokuwa anaishi.
Ghafla kipande kidogo cha karatasi nyeupe kikashuka mikononi mwake bila kuonekana kilikotokea. Doreen alicheka kwa sauti kali ya kutisha sana kisha akalikazia macho karatasi lile, matone ya damu yaliangukia kwenye karatasi lile kutoka kwenye macho yaliyotisha sana ya Doreen kwani yalikuwa na rangi nyeusi halafu yakawa na umbile kama macho ya paka.
"Nenda mpaka ofisi ya mkuu wa shule ukamalize kazi." alisema Doreen akiwa amelinyanyua karatasi like kwa mkono wake wa kushoto. Karatasi likatoweka mkononi mwake na kupepea kwa nguvu kama vile limerushwa na upepo mkali.
Doreen alipomaliza kazi hiyo akasimama vizuri kama mwanajeshi aliyejipanga kwaajili ya gwaride kisha akainamisha kichwa chake chini akapotea eneo lile.
****
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mabango walikuwa wanahofu kubwa sana kila wakikaa walifikiria kifo tu. Usingizi haukuwajia hata mara moja hivyo usiku waliketi makundi makundi wakizungumza hili na lile.
Wakati huo Dorice rafiki kipenzi wa Doreen alikuwa amejitenga pembeni akizungumza na mpenzi wake aitwaye Eddy, kijana mtanashati, mzuri, mpole na akili nyingi sana darasani.Wasichana wengi shuleni pale walitamani kuwa nae lakini bahati ilimwangukia Dorice pekee.
"Eddy unajua naogopa sana.." ilikuwa sauti ya Dorice akiwa amemkumbatia Eddy kwani kigiza kile cha usiku kiliwaficha wasionekane hivyo wakajiachia.
"unaogopa nini Dorice mpenzi wangu?"
"Naogopa kufa!" binti Huyo wa kinyaturu, mrembo aliyeumbika aliongea kwa sauti ya madeko sana.
"siku zote nakwambia Dorice kama Mungu alipanga huwezi kupangua , mwanadamu asikutishe kwa lolote. Huyu anayeua wenzake naye ipo siku yake tu maana hakuna atakae bakia milele na mwisho wa maji ni tope!"
"Najua mpenzi wangu ila hali kiukweli inatisha sana"
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mabango walikuwa wanahofu kubwa sana kila wakikaa walifikiria kifo tu. Usingizi haukuwajia hata mara moja hivyo usiku waliketi makundi makundi wakizungumza hili na lile.
Wakati huo Dorice rafiki kipenzi wa Doreen alikuwa amejitenga pembeni akizungumza na mpenzi wake aitwaye Eddy, kijana mtanashati, mzuri, mpole na akili nyingi sana darasani.Wasichana wengi shuleni pale walitamani kuwa nae lakini bahati ilimwangukia Dorice pekee.
"Eddy unajua naogopa sana.." ilikuwa sauti ya Dorice akiwa amemkumbatia Eddy kwani kigiza kile cha usiku kiliwaficha wasionekane hivyo wakajiachia.
"unaogopa nini Dorice mpenzi wangu?"
"Naogopa kufa!" binti Huyo wa kinyaturu, mrembo aliyeumbika aliongea kwa sauti ya madeko sana.
"siku zote nakwambia Dorice kama Mungu alipanga huwezi kupangua , mwanadamu asikutishe kwa lolote. Huyu aneua wenzake ipo siku yake tu!"
Akashtuka kidogo halafu akaichukua ili aisome vizuri. Mwalimu Mbeshi hakutaka kuamini kile alichokiona, akataharuki kwa hofu na mshangao mkubwa
ITAENDELEA SEHEMU YA TATU
Comments
Post a Comment